HATIMAYE UFARANSA YATUA FAINALI EURO 2016, USO KWA USO NA URENO


HATIMAYE UFARANSA YATUA FAINALI EURO 2016, USO KWA USO NA URENO

France fans

Wenyeji Ufaransa wamefanikiwa kufuzu kucheza hatua ya fainali ya Euro 2016 kwa ushindi wao wa kwanza dhidi ya Ujerumani kwenye michuano mikubwa tangu mwaka 1958.

Antoine Griezmann, ndiye mfungaji anayeongoza kwa magoli hadi sasa na ndiye aliyeamua mchezo huo kwa kufunga bao katika kila kipindi na kuipeleka Ufaransa kwenye mchezo wa fainali dhidi ya Ureno utakaochezwa Jumapili kwenye uwanja wa Stade de France.

Griezmann alianza kufunga mkwaju wa penati kipindi cha kwanza baada ya referee Nicola Rizzoli raia wa Italy kumtuhumun Bastian Schweinsteiger kuunawa mpira wakati akiwania mpira wa juu dhidi ya Patrice Evra.

Ufaransa iliweza kumudu presha ya Ujerumani kabla ya Griezmann kupachika bao la ushindi zikiwa zimesalia dakika 18 mpira kumalizika alipopiga mkwaju akiwa karibu na goli la Ujerumani kufuatia golikipa Manuel Neuer kuokoa krosi ya Paul Pogba.

Joshua Kimmich aligongesha mwamba kwa upande wa Ujerumani huku golikipa wa Ufaransa Hugo Lloris akiokoa mchomo wa hatari kuwanyima goli washindi hao wa kombe la dunia.

Rekodi zilizowekwa baada ya mchezo huo

  • Ufaransa ni nchi ya kwanza kufika fainali ya Euro ikiwa nchi mwenyeji wa mashindano (mara ya kwanza ilikuwa 1984)
  • Ufaransa wamefunga Ujerumani kwenye michuano mikubwa kwa mara ya kwanza tangu mwaka 1958. Ni mchezo wao wa kwanza pia kutoruhusu goli dhidi ya Ujerumani.
  • Ujerumani wamepoteza nusu fainali yao ya nne kati ya sita kwenye michuano mikubwa (2006, 2010, 2012, 2016).
  • Bastian Schweinsteiger amecheza mchezo wake wa 38 kwenye michuano mikubwa, michezo mingi zaidi ya mchezaji yeyote kwenye historia ya Kombe la Dunia na michuano ya Ulaya.
  • Michel Platini bado anashikilia rekodi ya magoli mengi zaidi kwenye msimu mmoja wa michuano ya Euro (magoli 9 Euro 1984) magoli matatu zaidi ya Antoine Griezmann aliyefunga magoli 6 hadi sasa Euro 2016


Comments