Mikel Arteta            amethibitisha kutundika daluga na kuweka wazi kuwa anakwenda            kuungana na benchi la ufundi la Manchester City chini ya Pep            Guardiola.
        Nahodha huyo wa            zamani wa Arsenal ametoa taarifa kupitia ukurasa wake wa            Twitter kuwa muda wake kama mchezaji umefika ukingoni na            anakwenda kufanya kazi na Guardiola. 
        "Kufutatia tetesi            nyingi za vyombo vya habari juu ya hatma yangu, sasa            ninathibitisha kuwa naondoka Arsenal na kwenda Manchester City            kama sehemu ya benchi la ufundi," aliandika Arteta.
        Mikel Arteta              amethibitisha kutundika daluga na kwenda kuwa kocha msaidizi               Manchester City 
        Hapa ilikuwa ni katika              mchezo wa mwisho wa Arteta kwa Arsenal mwezi Mei dhidi ya              Aston Villa ambapo alibubujikwa na machozi baada ya mpira              kumalizika
        Arteta anakwenda kuwa              msaidizi wa Pep Guardiola  
        
Comments
Post a Comment