HATIMAYE MANCHESTER UNITED YAKAMILISHA USAJILI WA PAUL POBGA KWA PAUNI MIL 100 ...atavaa jezi namba sita, mshahara pauni 290,000 kwa wiki


HATIMAYE MANCHESTER UNITED YAKAMILISHA USAJILI WA PAUL POBGA KWA PAUNI MIL 100 ...atavaa jezi namba sita, mshahara pauni 290,000 kwa wiki
Pogba was pictured at the Mr Chow restaurant in Los                Angeles on Thursday

Paul Pogba anatarajiwa kutambulishwa rasmi kama mchezaji wa Manchester United kufuatia kukamilika kwa uhamisho wake wa rekodi ya dunia wa pauni milioni 100.

WACHEZAJI 10 WANAOONGOZA KWA UHAMISHO WA BEI MBAYA DUNIANI

Paul Pogba - Juventus kwenda Man United £100m 

Gareth Bale - Tottenham kwenda Real Madrid £86m 

Cristiano Ronaldo - Man United kwenda Real Madrid £80m 

Gonzalo Higuain - Napoli to Juventus £76m 

Neymar - Santos kwenda Barcelona £72m

Luis Suarez - Liverpool kwenda Barcelona £63m

James Rodriguez - Monaco kwenda Real Madrid £60m 

Angel di Maria - Real Madrid kwenda Man United £60m 

Kaka - Milan to Real Madrid £56m

Kevin De Bruyne - Wolfsburg kwenda Man City£55m 

Taratibu za usajili wa Pobga unaomfanya arejee Old Trafford kwa mara ya pili, ulikamilishwa Alhamisi usiku.

Baada ya wiki kadhaa za majadialiano ya kina, United imekubaliana na ada ya Juventus kukamilisha usajili wa nne wa Jose Mourinho kiangazi hiki.

Pobga amekamilisha vipimo vya afya huko Los Angeles na atavaa jezi namba 6 Manchester United.

Dili hilo la usajili wa Pobga mwenye umri wa miaka 23, limekamilika baada ya wakala wake Mino Raiola kufanya maongezi na mawakili na maofisa wa Juventus Alhamsi mchana huko Turin. 

Hii inamaanisha kuwa mchezaji huyo aliyeondoka Old Trafford kama mchezaji huru mwaka 2012, anarejea akiwa mchezaji ghali anayevunja rekodi ya uhamisho ya Uingereza kwa pauni milioni 40.

Rekodi ya Uingereza ilikuwa inashikiliwa na Angel di Maria aliyenunuliwa na Manchester United kwa pauni milioni 60 kutoka Real Madrid.

United na Juventus zimekubaliana ada ya wakala Riola ambaye atahitaji asilimia 20 ya dili la Pobga.


Kiungo huyo wa kimataifa wa Ufaransa, anatarajiwa kulipwa mshahara wa pauni 290,000 kwa wiki.







Comments