HATIMAYE MANCHESTER UNITED YAKAMILISHA USAJILI WA PAUL POBGA KWA PAUNI MIL 100 ...atavaa jezi namba sita, mshahara pauni 290,000 kwa wiki
Paul Pogba            anatarajiwa kutambulishwa rasmi kama mchezaji wa Manchester            United kufuatia kukamilika kwa uhamisho wake wa rekodi ya            dunia wa pauni milioni 100.
        Taratibu za usajili            wa Pobga unaomfanya arejee Old Trafford kwa mara ya pili,            ulikamilishwa Alhamisi usiku.
        Baada ya wiki            kadhaa za majadialiano ya kina, United imekubaliana na ada ya            Juventus kukamilisha usajili wa nne wa Jose Mourinho kiangazi            hiki.
        Pobga amekamilisha            vipimo vya afya huko Los Angeles na atavaa jezi namba 6            Manchester United.
        Dili hilo la            usajili wa Pobga mwenye umri wa miaka 23, limekamilika baada            ya wakala wake Mino Raiola            kufanya maongezi na mawakili na maofisa wa Juventus Alhamsi            mchana huko Turin. 
        Hii inamaanisha            kuwa mchezaji huyo aliyeondoka Old Trafford kama mchezaji huru            mwaka 2012, anarejea akiwa mchezaji ghali anayevunja rekodi ya            uhamisho ya Uingereza kwa pauni milioni 40.
        Rekodi ya            Uingereza ilikuwa inashikiliwa na Angel di Maria aliyenunuliwa na Manchester            United kwa pauni milioni 60 kutoka Real Madrid.
        United na Juventus            zimekubaliana ada ya wakala Riola ambaye atahitaji asilimia 20            ya dili la Pobga.
        Kiungo huyo wa            kimataifa wa Ufaransa, anatarajiwa kulipwa mshahara wa pauni            290,000 kwa wiki.
        
Comments
Post a Comment