BAADA ya klabu              mbalimbali kuwania saini ya nyota wa Argentina, Gonzalo              Higuain aliyekuwa akihudumu SSC Napoli, hatimaye nyota huyo              ameamua kubaki katika serie A lakini akijiunga na miamba ya              kandanda, Juventus kwa kitita cha euro mil 94.
        Hatua hiyo              imezifanya klabu za Liverpool, Arsenal na Atletico Madrid              kusimama kumfukuzia nyota huyo mwenye miaka 28.
        Aidha hatua ya              Juventus kumnunua inatafsiriwa na wafuatiliaji wa mambo kuwa              huenda wapo njiani kumwachia kiungo wao, Paul Pogba atue              Manchester United huku wakimtaka kiungo wa Axel Witsel wa              Zenit kuziba pengo hilo.
        Nyota huyo              aliyekwenda nchini Hispania juma moja lililopita kwa ajili              ya kupima afya yake kwa ajili ya kujiunga na Biaconneri.
        Higuain amesaini              mkataba wa miaka minne ya kuitumikia miamba hiyo ya serie A              akizama hapo akiwa mchezaji bora wa msimu wa 2015/16.
        Msimu uliopita              nyota huyo wa zamani wa Real Madrid amefunga mabao 36 katika              serie A na kuiwezesha kucheza Ligi ya mabingwa msimu ujao.
        Hata hivyo,              mashabiki wa Napoli wamepania kumtendea visivyo Higuain pale              miamba hiyo itakapokutana Oktoba 30, mwaka huu kwenye mchezo              wa serie A msimu huu.
        
Comments
Post a Comment