NYOTA wa zamani              wa Barcelona, Hristo Stoichkov amedai kuwa nyota wa Real              Madrid, Cristiano Ronaldo huenda akatwaa tuzo ya Ballon d'Or              kutokana na mawazo yake ya kusema kuwa Antonio Griezmann na              Gareth Bale kama washindani.
        Griezmann na Bale              wanajiandaa kwa mechi za nusu fainali za Euro 2016 baada ya              kampeni nzuri walizofanya katika klabu zao za Atletico na              Real Madrid.
        Mfaransa              Griezmann amefunga mabao 32 katika michuano yote akiwa              Atletico, timu yake ikimaliza nafasi ya tatu La Liga na              kupoteza fainali Ligi ya Mabingwa kwa Real Madrid, wakati              Bale akiwa amefunga mara 19 na kutoa pasi 10 za goli.
        Lakini ikiwa ni              wiki moja tangu alipomtaja James Rodriguez wa Real Madrid              kama mchezaji wa kawaida sana, mkongwe huyo wa Bulgaria              aliamua kumzungumzia mshindi mara nne wa tuzo ya Ballon              d'Or, Ronaldo.
        "Griezemann ni              mchezaji hatari kwa kila mtu na ancheza soka matata sana,"              Stoichkov aliiambia radio ya Hispania Cadena Cope.
        "Lakini huenda              wakampa Cristiano Ronaldo tuzo hiyo tena kwa sababu ya              umbile lake zuri."
        Kuhusu Bale              ambaye atacheza dhidi ya Ureno leo, halikadhalika nae              akitarajiwa kuingia kwenye mbio za Ballon d'Or, Stoichkov              alisema mchawi huyo wa soka wa Wales atakuwa miongoni mwa              wanaowania tuzo hiyo iwapo Wales itatinga fainali Euro.
        
Comments
Post a Comment