KOCHA wa klabu ya              Manchester City, Claudio Ranieri amemtabiria kocha mpya wa              Manchester United kuwa atapata mafanikio kama aliyoyapata              kocha wa zamani wa âRed Devilsâ hao, Sir Alex Ferguson              ndani ya dimba la Old Trafford.
        Akiwa na kikosi              cha Leicester City, Ranieri alipewa nafasi moja kati ya 500              za kunyakua taji la Ligi Kuu England msimu uliopita na kwa              kile kilichoonekana kama maajabu mapya ya soka, Leicester              ilibeba taji hilo kwa mara ya kwanza ndani ya miaka 132              tangu klabu hiyo ianzishwe.
        Mourinho              alinyakuliwa na United na kupewa mkataba wa kuinoa timu hiyo              iliyokuwa chni ya Mholanzi Louis Van Gaal msimu uliopita na              Ranieri anaamini Mreno huyo ana nafasi ya kufanya vizuri              msimu ujao kwenye Ligi Kuu England.
        âMourinho ana              uwezo wa kuwa Ferguson mpya,â alisema Ranieri.
        âAtadumu United              kwa miaka 26 lakini ataacha alama ya ushindi.â
        Upinzani bainia              ya Ranieri na Mourinho unategemewa kuwa mkali msimu ujao.              Sambamba na makocha wengine waliotua England, Antonio Conte              (Chelsea) na Pep Guardiola (Man City).
        
Comments
Post a Comment