KOCHA mpya wa miamba ya soka ya              Ujerumani, Bayern Munich, Carlo Ancelotti amewaahidi              mashabiki wake kuwa atakuwa na mchezo wa kuvutia na              kushambulia.
        Kama ilivyokuwa mtangulizi weake, Pep              Guardiola, Ancelotti alianza kuzungumza Kijerumani kabla              hajaendelea na Kiitaliano na Kiingereza wakati wa maswali na              majibu.
        Guardiola ameshinda mataji matatu ya              Bundesliga kabla hajaamua kuachana na kuinoa miamba hiyo.
        Ancelotti anatarajiwa kuwaletea Bayern              taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya kutokana na kuwa na historia              nzuri akitoka kuinoa AC Milan na baadae Real Madrid.
        Hata hivyo, mwenyekiti wa klabu hiyo,              Karl-Heinz Rummenigge na Ancelotti hawana nia ya kupunguza              wala kuongeza wachezaji.
        
Comments
Post a Comment