BUFFON "AWAKA" AKIKATAA KULINGANISHWA NA MANUEL NEUER



BUFFON "AWAKA" AKIKATAA KULINGANISHWA NA MANUEL NEUER
KIPA mkongwe na nahodha wa heshima wa Italia, Gianluigi Buffon ameibuka na kuwajia juu wanaotaka kumlinganisha na kipa wa Ujerumani, Manuel Neuer.

Buffen, 38, aliisaidia Italia kutwaa ubingwa wa dunia mwaka 2006 na anashikilia rekodi ya kuwa kipa ghali zaidi duniani alipotua Juventus akitokea Parma kwa pauni mil 33 mwaka 2001.

Kipa huyo ameweza kuipa lundo la mataji Juventus tangu atue kikosini hapo ambapo wametwaa mataji kibao ikiwemo ubingwa wa serie mfululizo.

Neuer ndiye kwanza nae ameanza kuhesabu mafanikio ambapo mwaka 2014 aliipa ujerumani Kombe la Dunia, tayari ametwaa tuzo kadhaa za akiwa na Bayern Munich.

Lakini Buffon ambaye amemwelezea Neurer kma kipa bora kwa sasa, amekataa katakata kulinganisha nae kwa kiwango cha sasa.

"Nimesema Neuer ni zaidi yangu kwasababu bado ana nafasi ya kufikia na kupita mafanikio yangu baadae, hilo sio jambo la kunikwaza kuangalia mimi niko vipi."

"Najijua nilivyokuwa, nilivyo kwa sasa na wapi nitakuwa kwa miaka miwili ijayo. Hii inanifanya niamini atapata mafanikio zaidi siku zijazo," alisema.


Alionya kuwa ni kosa la jinai kumlinganisha na kipa huyo mwenye miaka 30 ambaye bado anakipiga.


Comments