BAADA ya klabu ya              Manchester United kutangaza namba mpya za jezi za wachezaji              wao kwa ajili ya msimu wa 2016/17, sasa mtafaruku mkubwa              umezuka baada ya Zlatan Ibrahimovic kupewa jezi namba tisa              iliyokuwa ikitumiwa na kinda Anthony Martial.
        Tayari              ilishajulikana wazi kuwa Ibrahimovic angevaa jezi hilo,              lakini tangazo la kubadilishwa kwa namba lilitolewa wakati              Martial akiwa bado kwenye mapumziko yake, jambo              lililoonekana kutomridhisha Mfaransa huyo aliyeamua              kuonyesha hasira zake kwenye mtandao wa kijamii.
        Matrtial aliamua              kufuta urafiki na akaunti rasmi ya Manchester United katika              mtandao wa Twitter kutoka ile iliyokuwa ikimuonyesha              akishangilia bao na kuweka picha aliyopiga ikiwa na jina              lake sambamba na namba tisa.
        United ilimsajili              mshambuliaji huyo mwaka jana kwa dau linalotabiriwa kupanda              hadi euro mil 80 na sasa imemkera kwa kumbadilisha namba na              kumpa jezi namba 11 bila ridhaa yake, huku ikidaiwa kuwa              huenda hiyo ikawa changamoto ya kwanza atakayokutana nayo              Jose vyumba vya kubadilisha nguo.
        
Comments
Post a Comment