ZIDANE AITAKA REAL MADRID IMSAJILI N'GOLO KANTE WA LEICESTER CITY



ZIDANE AITAKA REAL MADRID IMSAJILI N'GOLO KANTE WA LEICESTER CITY REAL MADRID imeingia katika mbio za kusaka saini ya N'Golo Kante wa Leicester, hii ni kwa mujibu wa ripoti kutoka Hispania.
GETTY
Gazeti la Marca la Hispania limedai kuwa kocha wa Real Madrid Zinedine Zidane ameiagiza klabu yake kufanya kila wawezalo ili kumsajili kiungo huyo wa kimataifa wa Ufaransa.
Zidane  anataka kuboresha safu yake ya kiungo cha ukabaji katika kipindi hiki ambacho  Casemiro yuko peke yake kwenye eneo hilo.
Kante alijiunga na Leicester kwa pauni milioni 5.6 kiangazi kilichopita akitokea Caen ya Ufaransa.


Comments