UNAWEZA kusema ni              kama kapagawishwa, straika Wayne Rooney amekiangalia kikosi              cha timu ya taifa ya England kitakachokwenda kucheza kwenye              michuano ya fainali za Mataifa ya Ulaya "Euro 2016" na kisha              akasema kuwa anavyoona ndicho bora tangu aanze kuitumikia              timu hiyo.
        Nahodha huyo na              mfungaji bora, alianza kuichezea timu hiyo Februari, 2003 na              tayari ameshaichezea katika mashindano makubwa matano na              huku ya sita yakiwa njiani.
        Hata hivyo Rooney              mwenye umri wa miaka 30 anasema kuwa, anavyoamini kikosi cha              sasa atakachosafiri nacho kwenda Ufaransa kinavipiku vyote              vilivyopita lakini akasema kuwa wanatakiwa kujifunza kutoka              kwa wapinzani.
        "Kikosi hiki kina              kila kitu cha kuwa bora tofauti na vingine nilivyowahi              kuvichezea," staa huyo aliwaambia waandishi wa habari.
        "Nadhani hatma ya              kikosi cha England sasa ipo wazi. Unaweza kufanya vizuri              majira haya ya joto," aliongeza nyota huyo.
        Alisema kwamba              anavyofahamu wana kikosi kizuri lakini wanachotakiwa kufanya              ni kujituma.
        
Comments
Post a Comment