KIWANGO bora              kilichoonyeshwa na timu ya taifa ya Wales, kimefanya              wachambuzi wengi wa soka kubadili mitazamo yao na sasa              wanaipa nchi hiyo nafasi ya kutinga fainali.
        Wales ambayo              haikuwa ikipewa nafasi na wengi, imeonyesha soka la hali ya              juu ambapo imepoteza mchezo mmoja na kushinda miwili katika              hatua ya makundi na hivyo kuwa kinara wa Kundi B. 
        Hata hivyo              mashindano ya mwaka huu yameelezwa kukosa msisimko kutokana              na hofu ya mashambulizi ya kigaidi pamoja na mfungo wa mwezi              mtukufu wa Ramadhani.
        Ufaransa ni moja              ya ncchi za Ulaya zenye waislamu wengi, hivyo inaaminika              kuwa mashabiki wengi waislamu wa ndani na nje ya Ufaransa,              wamejizuia kuungana na mashabiki wengine kushuhudia michuano              hiyo, badala yake wamebaki majumbani wakifanya ibada zaidi              katika mwezi huu.
        
Comments
Post a Comment