Video: RONALDO ALIVYOWAZUIA ASKARI KUMKAMATA SHABIKI ALIYETAKA KUPIGA ‘SELFIE’


Video: RONALDO ALIVYOWAZUIA ASKARI KUMKAMATA SHABIKI ALIYETAKA KUPIGA 'SELFIE'

Ronaldo-shabiki

Licha ya machungu ya kushindwa kupata ushindi kwenye mchezo wa Ureno vs Austria, superstar wa Real Madrid na timu ya taifa ya Ureno Cristiano Ronaldo aliwazuia walinzi wa uwanja waliokuwa wanataka kumwondosha shabiki aliyevamia uwanjani na kupiga naye selfie.

Baada ya mchezo kumalizika, ghafla shabiki alishuka toka jukwaani na kuvamia uwanjani kisha kumwelekea Ronaldo akitaka kupiga naye picha 'selfie'. Walinzi wa uwanjani wakamkimbilia shabiki huyo na kutaka kumtoa uwanjani lakini Ronaldo aliwazuia kisha kupozi na shabiki huyo kwa ajili ya picha.

Wakati mashindano ya Euro yakiendelea, nchini Ufaransa kumekuwa na hali ya wasiwasi huenda matukio ya kigaidi yakatokea katika kipindi hiki. Ulinzi umekuwa ukiimarishwa kila kukicha lakini bado matatizo madogomadogo yamekuwa yakijitokeza.

Kila mtu amekuwa akifurahia hali ya utulivu ya sasa huku kukiwa hakujaripotiwa vurugu za mitaani pamoja na urushaji wa mafataki uwanjani, shabiki huyo alijitosa uwanjani na kuwaacha watazamaji wakisubiri kuona walinzi watachukua hatua gani.

Hii hapa video inayokupa fursa ya kushuhudia tukio zima



Comments