Usiku wa kuamkia leo,                mitanange mitatu ilikanyagwa katika viwanja 3 tofauti.
        Mchezo wa kwanza uliwa                shuhudia Peru wakiwafunga Haiti goli 1-0. Kipindi cha                kwanza hakikuwa na goli ingawa Peru walimiliki zaidi mpira                hasa katikati ya uwanja wakitumia mfumo wa 4-4-2 na                kuwabana Haiti ambao wao walitumia mfumo wa 4-3-3.
        Iliwachukuwa Peru mpaka                dakika ya 66 kujipatia bao lao lililowekwa kimiani na                mshambulizi hatari Paolo Guerrero kwa kichwa cha kuchumpa                kufuatia krosi mujarabu iliyotumwa na Edson Flores na                kumshinda golikipa Johny Plaside wa Haiti. Haikushangaza                Guerrero kufunga bao hili kwani ikumbukwe kuwa huyu ndiye                mfungaji bora wa mashindano haya kwa misimu miwili                iliyopita.
                COSTA RICA vs PARAGUAY
        Wengi walitarajia kuwa                mpambano huu utakuwa wa mbinu za kutafuta mabao pamoja na                ufundi mkubwa, lakini tofauti yake ikawa ni mtanange wa                nguvu zaidi na kukamiana, kitu kilichopelekea mwanuzi                kugawa kadi kama njugu, kwani alitoa kadi za njano kwa                wachezaji 5 kadi nyekundu kwa mchezaji wa Costa Rica                Kendall Waston mnamo dakika ya 94.
        
BRAZIL vs EQUADOR
        Katika kipute hiki                matokeo yalikuwa ni kutofungana (0-0), lakini ukweli ni                kuwa huu ulikuwa ni mchezo uliokuwa wa kuburudisha (very                entertaining) kuliko michezo mingine yote iliyokwisha                kuchezwa hadi sasa. Kwa upande wa Brazil waliotumia mfumo                wa 4-2-1-2-1 na kuwatumia zaidi Willian Coutinho                kuchezesha timu, walipeleka sana mashambulizi langoni mwa                Equador lakini kipa wa Equador aliweza kuokoa hatari zote.
        Mnamo dakika ya 66 ya                mchezo, mchezaji hatari wa Equador Miller Balanos alimpita                golikipa wa brazil pembeni ya lango na kuuweka mpira                kimiani, lakini mwamuzi alilikataa bao hilo kwa madai                mpira ule ulikuwa umetoka kabla mfungaji hajaitia kambani.                Hivyo mpaka mwisho matokeo ni 0-0.
        Leo usiku kuamkia kesho
        JAMAICA vs VENEZUELA                (Soldier Field)
        MEXICO vs URUGUAY                (Phoenix Stadium)
        

Comments
Post a Comment