SUAREZ AMKOROMEA KOCHA NA KUMALIZIA HASIRA ZAKE KWA KUPIGA NGUMI UZIO WA BENCHI URUGUAY IKIAGA COPA AMERICA ...kocha wake anena



SUAREZ AMKOROMEA KOCHA NA KUMALIZIA HASIRA ZAKE KWA KUPIGA NGUMI UZIO WA BENCHI URUGUAY IKIAGA COPA AMERICA ...kocha wake anena
Luis            Suarez hits the dugout in frustration after finding out he had            not been named as a sub during the game 

Luis Suarez ameshindwa kuzuia hasira zake na kuishia kulipiga kwa ngumi benchi la wachezaji wa akiba katika mchezo wa Copa America dhidi ya Venezuela.

Hakuchezeshwa katika mchezo huo wa kipigo cha kuduwaza cha 1-0 na kupelekea Uruaguay kuaga michuano hiyo baada ya kufungwa pia 3-1 na Mexico katika mchezo wao wa kwanza.

Goli la Salomon Rondon la kipindi cha kwanza likatosha kuimaliza Uruguay huku karibu muda wote wa mchezo Suarez akiamini kuwa ataingizwa uwanjani kuikoa nchi yake.

Hata hivyo ilibainika baadae kuwa licha ya Suarez kupasha mwili moto na wenzake kabla ya mchezo, lakini jina lake halikuwepo hata kwenye wachezaji wa akiba.

Wakati mashabiki walipokuwa wakiimba jina lake kutaka aingizwe, Suarez ambaye hakucheza pia katika mchezo wa kwanza, aliinuka na kupasha mwili lakini kocha  Oscar Tabarez alipoanza kufanya mabadiliko, mshambuliaji huyo hakuitwa.

Kwanza aliitwa aliingizwa Diego Rolan, baadae Nicolas Lodeiro na mwishowe  Matias Corujo hatua iliyopekea Suarez kwenda kumkoromea kocha wake na kupiga uzio wa benchi.

Lakini hakukuwa na namna, Suarez asingeweza kucheza mchezo huo kwa kuwa jina lake halikujumuishwa kwenye orodha ya wachezaji wa akiba. Pengine hakufahamishwa hilo.

Kocha Tabarez akasema baada ya mchezo: "Suarez hayuko tayari kucheza, hiyo ni juu ya madaktari.   Hata imkere kwa kiasu gani - na hakunieleza kitu chochote - sitamchezesha mchezaji ambaye hayuko fiti kwa asilimia 100".
Luis Suarez hits the dugout                  in frustration after finding out he had not been named                  as a sub during the game 
Luis Suarez akipiga uzio wa benchi kwa hasira
The Barcelona star looks                  dejected after realising he would not be coming off the                  bench against Venezuela
Nyota wa Barcelona akiwa mnyonge kwenye benchi
Suarez warmed up with his                Uruguay team-mates before the match but was not included                as a substitute 
Suarez alipasha mwili na wachezaji wenzake wa Uruguay kabla ya mchezo na Venezuela
Suarez, who missed Uruguay's                  defeat by Mexico, had expected to be given a chance as                  his side chased a goal
Suarez, ambaye pia alikosa mchezo dhidi ya  Mexico akipashwa mwili moto lakini hakuingizwa dimbani
Salomon Rondon celebrates after giving Venezuela the                lead against Uruguay in their Copa America clash
Salomon Rondon akishangilia bao lake


Comments