KIUNGO wa Ufaransa na Juventus                  anayehusishwa na usajili wa kurejea Manchester United,                  Paul Pobga amesema hajutii kitendo chake alichokifanya mwaka 2012 cha kumwambia Alex Ferguson kuwa anataka kuondoka                  Old Trafford.
              Akizungumza kwenye kambi ya Ufaransa                  inajiandaa na Euro 2016, Pobga alisema: "Ni kocha                  ninayemheshimu sana. Lakini yeye ni binaadamu. Mimi huwa                  sisiti kusema kile ninachokifiria. Iwe ni Ferguson au                  Barack Obama nitasema tu.
              "Ferguson alinifuata, tukazungumza.                  Alitaka nibaki United, lakini tayari nilikuwa na maamuzi                  yangu."
              Pobga anatajwa kuwaniwa na Manchester                  United kwa pauni milioni 78.
              Pogba alisaini Juventus              baada ya kuondoka United na kufanikiwa kushinda mataji mengi              Italy
        Pogba (katikati)              aliondoka United mwaka 2012 akiwa amecheza mechi tatu za              kikosi cha kwanza
          
Comments
Post a Comment