MIRAELM            Pjanic amekamilisha usajili wake kutoka Roma na kujiunga na            Juventus, hivyo kuziacha solemba Chelsea na Manchester United            zilizokuwa zikimtolea macho.
        Kocha            ajaye Chelsea, Antonio Conte aliripotiwa kunuia kumpeleka            kiungo huyo Stamford Bridge sambamba na mchezaji mwenzake            Radja Nainggolan, huku Jose Mourinho naye akielezwa kumfanya            Mbosnia huyo wa miaka 20 kuwa moja ya malengo yake Old            Trafford.
        Pjanic aliwasili Turin kufanyiwa vipimo vya afya mapema            Jumatatu, kisha akajiunga na klabu hiyo kwa dau la pauni            milioni 25 akisaini mkataba wa miaka mitano.
        
Comments
Post a Comment