MANCHESTER United imeweka mezani ofa ya            pauni milioni 35.2 kwa ajili ya kumsajili kiungo wa kati wa            Valencia, Andre Gomes katika dirisha la usajili wa kiangazi            hiki.
        Gomes alifunga mabao tisa katika mechi 77            alizoichezea Valencia tangu alipoichezea kwa mara ya kwanza            timu hiyo ya La Liga mwaka 2014, lakini staa huyo wa miaka 22            sasa anahusishwa kwa nguvu na kuhamia Old Trafford.
        Mwandishi wa habari wa Italia anayesifika            kwa kuandika habari zenye ukweli, Alfredo Pedulla ameripoti            kuwa United imeweka mezani pauni milioni 35.2 kwa ajili ya            Mreno huyo, pamoja na bonasi ya pauni milioni 11.7.
        Jose Mourinho yupo katika harakati za            kuiongezea nguvu safu ya kiungo ya United baada ya kukabidhiwa            mikoba ya kuinoa timu hiyo mwishoni mwa Mei.
        Inaeleweka kuwa mwakilishi wa Gomes, Jorge            Mendes ambaye pia ni wakala wa Mourinho atasaidia kusukuma            mchakato wa kufanikisha dili hilo.
        
Comments
Post a Comment