MANCHESTER CITY imejitoa katika mbio za            kumuwania kiungo wa Juventus, Paul Pogba hivyo kutoa nafasi            kwa Manchester United kumrejesha kundini staa huyo raia wa            Ufaransa.
        Kwa mujibu wa gazeti la Manchester Evening            News, kocha mpya wa City, Pep Guardiola ameliondoa jina la            kiungo huyo katika orodha yake ya wachezaji anaowataka katika            dirisha hili la usajili wa kiangazi.
        Kutokana na ripoti hiyo, sasa Jose            Mourinho anaweza kuweka mezani dau rekodi kwa England kwa            ajili ya staa huyo wa miaka 23 katika harakati zake za kusuka            kikosi kitakachompa taji la Premier League katika msimu wake            wa kwanza Old Trafford.
        Pogba amekuwa akihusishwa na uhamisho wa            pauni milioni 60 kurudi katika klabu yake ya zamani,            aliyoondoka mwaka 2012 baada ya kukosa uwezekano wa kucheza            kikosi cha kwanza.
                                        
Comments
Post a Comment