Luiz Felipe Scolari            anataka kuwa kocha mpya wa England, nafasi ambayo aliikataa            miaka kumi iliyopita.
        Scolari, 67,            alikataa kuwa mrithi wa Sven            Goran Eriksson mwaka 2006 baada ya FA kuweka hadharani utashi            wao huo huku akiwa bado yupo kwenye mkataba wa kuifundisha            Ureno.
        Lakini baada ya Gareth Southgate kuweka wazi kuwa hana            mpango wa kumrithi Roy Hodgson            katika mkataba wa kudumu na kwamba anachoweza kufanya ni kuwa            kocha wa muda tu, Scolari ameibuka            na kusemma anaitaka nafasi hiyo.
        Scolari, ambaye kwa            sasa anafanya kazi China, ameiambia Daily Mail la            Uingereza: "Kwasasa mimi ni kocha wa Guangzhou na ninaizingatia kazi yangu hapa.            Lakini najua  umuhimu wa kibarua cha England katika ulimwengu            wa soka.
        "Najua umuhimu wa            kuwa kocha wa taifa kupitia muda wangu niliokuwa mwalimu wa            Brazil na Ureno."
        
Comments
Post a Comment