MANCHESTER United wanaandaa uwezekano wa              kufanya uhamisho mkubwa wa kumsajili straika wa Barcelona,              Lionel Messi.
        Gazeti la Daily Mail la Uingereza              limeripoti kuwa, United imetuma maombi mara mbili katika              wiki tatu zilizopita katika jaribio la kumsajili Muargentina              huyo.
        Uhamisho wowote unaonekana kulenga              kuirejesha United katika Ligi ya Mabingwa Ulaya chini ya              Jose Mourinho msimu wa 2017/18.
        Usajili wa Messi unaweza kuvunja rekodi              ya pauni mil 85.3 ambazo Real Madrid walilipa kwa Tottenham              ili kumnasa Gareth Bale.
        Mkataba wa sasa wa Messi Nou Camp              unatarajiwa kumalizika 2018 na imebainika kuwa anahitaji              kuhakikishiwa mambo kadha kama wanataka kumbakisha Barcelona              ambapo amefunga jumla ya mabao 453 katika mechi 531.
          
            
        United imekuwa ikisaka mchezaji mwenye              jina kubwa na ishajaribu kumsajili Cristiano Ronaldo hivi              karibuni, wakati pia ishajaribu kuwanasa Bale na Neymar              mwaka jana.
        
Comments
Post a Comment