EURO 2016: URENO YA RONALDO YASHINDWA KUTAMBA KWA ICELAND ....Austria nayo yachapwa 2-0 na Hungary




EURO 2016: URENO YA RONALDO YASHINDWA KUTAMBA KWA ICELAND ....Austria nayo yachapwa 2-0 na Hungary
URENO imeanza vibaya kampeni zake za kusaka taji la Euro 2016 baada ya kulazimishwa sare na timu isiyopewa nafasi - Iceland.

Luis Nani aliifungia Ureno bao la kuongoza dakika ya 31 lakini Bjarnason akaisawazishia Iceland dakika ya 50 wakati supastaa wa Ureno Cristiano Ronaldo akipoteza nafasi ya wazi ya kuifungia nchi yake bao la ushindi.

Ukingoni mwa mchezo, Nani alimtumia Ronaldo krosi tamu akiwa ndani ya sita lakini Ronaldo ambaye anaweza kuwa ndiye mfungaji bora wa magoli ya vichwa barani Ulaya, akaishia kupiga mpira uliokwenda mikononi mwa kipa Hannes Halldorsson.

Katika mchezo mwingine Austria ikachapwa 2-0 na Hungary kwa magoli yaliyofungwa na  Adam Szalai na  Zoltan Stieber.
Nani                  celebrates after giving Portugal the lead in the                  evening's second Group F fixture against Iceland at                  the Geoffroy-Guichard stadium
Nani akishangilia goli lake
Nani                  slots the ball home with a neat side-footed finish to                  put the favourites, led by Cristiano Ronaldo, ahead in                  the first-half
Nani akipiga mpira uliokwenda wavuni
Vieirinha falls to the floor after missing a cross                  to the back post as Bjarnason fires the ball into the                  net past a helpless Rui Patricio
Vieirinha anaserereka chini baada ya kuukosa mpira na kuruhusu  Bjarnason wa Iceland afunge kirahisi
Bjarnason jumps for joy and celebrates Iceland's                  first-ever goal in European Championship history as his                  team-mates race to join him
Bjarnason akiruka juu na kushangilia goli la kwanza kwa Iceland katika historia ya michuano ya Ulaya



Comments