DAVID DE GEA amekumbwa na kashfa ya            ngono iliyotishia kutimuliwa kwenye timu ya taifa ya Hispania            inayoshiriki michuano ya Euro 2016.
        Kipa huyo wa Manchester United jina            lake limetajwa mahakamani na shahidi aliyedai kuwa De Gea            alishiriki mahusiano na changudoa bila ridhaa yake.
        Hata hivyo De Gea amekanusha vikali            na kusema jambo hilo linashughulikiwa na mawakili wake. 
        De Gea amesema katika            mkutano na waandishi wa habari: "Yote ni uongo. Najisikia mwenye nguvu zaidi kubakia timu            ya taifa... habari hizo si za kweli na ipo mikononi mwa            wanasheria wangu.
        "Sikuwahi kufikiria suala            la kuondoka timu ya taifa. Inanipa ari ya kufanya mazoezi kwa            nguvu zaidi".
        Tuhuma hizo zinasema            mwaka 2012 kipa huyo namba moja wa United aliandaa  mipango ya            'mechi' hiyo ya ngono kwaajili ya mchezaji mwenzake wa U-21 ya            Hispania Iker Muniain pamoja na            mchezaji mwingine ambaye hakutajwa jina dhidi ya changudoa            bila ridhaa yake.
        Tovuti moja              ya Hispania El Diario inasema madai hayo            yalikuwa sehemu ya ushahidi uliotolewa kwa waendesha mashtaka            katika kesi ya mfanyabishara wa danguro la ngono Torbe ambaye jina lake            halisi ni Ignacio            Allende Fernandez. 
        Torbe alibakia rumande mwezi            April baada ya kukutwa na hatia ya kuendesha biashara ya            ukahaba kwa kutumia wasichana wenye umri mdogo.
        Shahidi aliyetambulika kama            TP3 akadai De Gea aliandaa mkutano na Torbe kwa niaba ya Muniain na mchezaji mwingine            katika hotel ya nyota tano jijini Madrid mwaka 2012.
        Mpelelezi              wa Kihispania ameripotiwa akisema anaamini katika ushahidi              uliotolewa na TP3 pamoja na wanawake wengine wawili              waliohojiwa katika utaalamu wa hali ya juu.
        Ripoti ya              polisi iliyotolewa Juni 3, 2015 ilisema: "Baada ya kumwacha              mwanamke huyo chumbani pamoja na msichana mwingine, Torbe              alimwambia wanapaswa kulalala na wanasoka na kukubali              kufanya kila watakalotaka na kwamba hatua hiyo ingewaingizia              kipato kikubwa.
        
Comments
Post a Comment