CHRISTIAN BENTEKE amesema anataka kubaki Liverpool lakini ataondoka iwapo hatakuwepo kwenye mipango ya kocha Jurgen Klopp.
Mshambuliaji huyo alisajiliwa kwa pauni milioni 32.5 kutoka Aston Villa kiangazi kilichoipita lakini akashindwa kuonyesha makali yake.
Alifunga magoli 10 tu katika michezo 42 aliyocheza na mara nyingi akawa akitokea benchi kufuatia ujio Klopp mwezi Oktoba.
Bosi huyo wa            Kijerumani alipendelea zaidi kuwatumia Divock Origi, Daniel            Sturridge au Roberto Firmino kwenye safu yake ya ushambuliaji.
        "Bado nina mkataba hapa na ningependa kubaki iwapo kocha ataniweka kwenye mipango yake"Christian Benteke
Benteke ambaye bado            ana miaka minne kwenye mkataba wake Liverpool, ataamua hatima            yake baada ya Euro 2016.
        "Katika umri wangu            huu wa miaka 25 , sio kijana wala mzee lakini ni muhimu            kucheza", alisema Benteke nyota wa kimataifa wa Ubelgiji.
        "Bado            nina mkataba pale na ningependa kubaki iwapo kocha ataniweka            kwenye mipango yake.
        "Kama haitakuwa hivyo, itakuwa            vigumu kwangu kubakia Liverpool. Nitafikiria zaidi baada ya            Euro," alisema katika mkutano wa waandishi wa habari.
        
Comments
Post a Comment