TIMU ya Borussia              Monchengadbach imemtia kitanzi staa wake, Raffael ambapo              itashuhudiwa akiendelea kuitumikia klabu hiyo hadi mwaka              2019.
        Mkataba wa sasa              wa straika huyo mwenye umri wa miaka 31 ulitarajiwa              kumalizika mwakani lakini sasa amefikia makubaliano ya              kuendelea kuitumikia klabu hiyo ya Bundesliga.
        Raffael alijiunga              na klabu hiyo ya Borussia Park mwaka 2013 akitokea katika              timu ya Dynamo Kiev na hadi sasa ameshafunga mabao 44 katika              mechi 116 alizoichezea katika mashindano yote.
        Msimu uliopita              staa huyo raia wa Brazil alifunga mabao 13 na kutoa pasi za              mwisho 10 katika mechi 31za Ligi.
        Walikuwa ni              wachezaji Robert Lewandowski, Pierre-Emerick Aubameyang,              Henrikh Mkhitaryan na Thomas Muller ambao walimzidi mabao              kwenye michuano hiyo ya Bundesliga.
        
Comments
Post a Comment