BARCELONA NA REAL MADRID VITANI KUSAKA SAINI YA KIUNGO WA LIVERPOOL



BARCELONA NA REAL MADRID VITANI KUSAKA SAINI YA KIUNGO WA LIVERPOOL
GETTY
BARCELONA na Real Madrid zote ziko vitani zikisaka saini ya kiungo wa Liverpool Cameron Brannagan.

Kinda huyo wa miaka 20 alikuwa na wakati mzuri Anfield msimu uliopita ambapo alicheza mmechi tisa tangu alipocheza mechi yake ya kwanza mwezi Septemba.

Mwezi April gazeti la Hispania Sport lilidai Barcelona imekuwa ikimfuatilia Brannagan ikiwa imedhamiria kuongeza wachezaji vijana kwenye kikosi chake.
Lakini Daily Mirror la Uingereza limeibuka na kusema Real Madrid nayo inasaka saini ya kiungo huyo chipukizi wa England.



Comments