Lionel Messi ameifikia                rekodi ya Gabriel Batistuta (Bat Goal) ya kuwa mfungaji wa                wakati wote kwa timu ya taifa ya Argentina baada ya                kuifungia timu yake bao na kufikisha mabao 54. Messi                aliiongoza Argentina kuichapa Venezuela mbao 4-1 na kufuzu                nusu fainali kwa kupambana na wenyeji Marekani.
        Argentina walianza                kujipatia ushindi dakika ya 8 tu pale Gonzalo Huguain                alipopachika mpira kimiani kufuatia pande safi alilomegewa                na Messi. Dakika 20 baadaye yaani dakika ya 28 Gonzalo                Huguain akaipatia timu yake bao la pili. Mnamo dakika ya                43 mwamuzi Roberto Orozco akawazawadia Venezuela penati,                ambapo mchezaji Seijas alipiga kwa staili ya "Panenka il                Cucchiais" lakini kipa wa Argentina Romelo aliishitukia na                kutulia pale pale na kuidaka.
        Dakika ya 60 ndipo                'Rapulga' Lionel Messi akaifungia timu yake bao la 3.                Venezuela walijipatia goli la kifuta chozi dakika ya 70                kupitia kwa nyota wake Solomoni Rondon, goli ambalo                halikudumu hata dakika 1 kwa dakika ya 71 Lamela akaipatia                Argentina bao la 4.
                Nako kwenye dimba la                Levis Stadium,Santa Clara Califonia, Chile walimpa Mexico                mapumziko ya wiki yaani goli 7-0.Alikuwa mchezaji hatari                wa Chile Eduardo Vargas aliyeingia kimiani mara 4, dakika                ya 15, 51, 56 na 73.Huku Edson Puch akifunga goli 2,                dakika ya 44 na 86, naye Alexis Sanchez akifunga goli moja                dakika ya 48. Sasa Chile atapambana na Colombia katika                hatua ya nusu fainali.
        

Comments
Post a Comment