STRAIKA wa klabu              ya Atletico Madrid na Ufaransa, Antoine Griezmann amesema              ana uhakika kuwa kiungo Paul Pogba ana uwezo mkubwa wa kuwa              mchezaji bora wa dunia. 
        Griezmann              aliongeza kuwa nyota huyo wa klabu ya Juventus atakuwa              msaada mkubwa kwa taifa la Ufaransa katika kuhakikisha              wanatwaa Kombe la Euro litakalofanyika kwenye ardhi yao.
        "Ana nguvu na              ubunifu mkubwa sana, kasi na uwezo kubwa wa kupiga mashuti,              nafikiri Pogba ana kila sifa ya kuwa nyota wa dunia,"              alisema Griezmann.
        
Comments
Post a Comment