BEKI wa zamani wa              Chelsea William Gallas amemtaka kocha mpya wa klabu hiyo,              Antonio Conte kuinusuru klabu baada ya kushindwa kufanya              vizuri msimu uliopita ambapo ilishindwa kutetea ubingwa wake              na kumaliza ikiwa nafasi ya kumi.
        Aliyekuwa kocha              wa timu hiyo, Jose Mourinho ndie aliyetolewa kafara kwa              kufukuzwa Desemba mwaka jana, kabla ya Guus Hiddink              kuinusuru isishuke daraja.
        Conte ndie              atakaeinoa klabu hiyo ya tanford Bridge baada ya kuiongoza              Italia kwenye michuano ya fainali za Mataifa ya Ulaya Uero              2016 na Gallas ambaye amewahi kutwaa ubingwa wa Ligi Kuu              mara mbili akiwa na Chelsea katika kipindi cha 2001 na 2006              alichoitumikia ana matumaini kocha huyo wa zamani wa              Juventus ataiwezesha kurejea kileleni mwa msimamo wa Ligi.
        "Ni vigumu mno              kuinoa Chelsea ikiwa kwenye nafasi kama hii hususan katika              kipindi cha miaka mitano niliyokuwa mahali hapo," beki huyo              wa zamani wa Ufaransa aliuambia mtandao wa Omnisport.
        "Lakini inaweza              ikatokea kwa klabu kubwa kama hii, nadhani msimu ujao              utakuwa mwingine, nina matumaini tutaiona Chelsea ikiwa              kileleni," alisema staa huyo wa zamani.
        
Comments
Post a Comment