WAZIRI MKUU WA ITALIA AMPONGEZA CLAUDIO RANIERI BAADA YA LEICESTER KUTWAA UBINGWA ENGLAND



WAZIRI MKUU WA ITALIA AMPONGEZA CLAUDIO RANIERI BAADA YA LEICESTER KUTWAA UBINGWA ENGLAND
Claudio Ranieri            arrives at Leicester's training ground on Tuesday after            winning the Premier League title

WAZIRI MKUU wa Italia, Matteo Renzi, amempongeza Claudio Ranieri (pichani juu) baada ya kushinda taji la Premier League akiwa na Leicester City Jumatatu usiku.

Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Renzi aliandika kuwa "mafanikio makubwa zaidi katika historia ya soka la England yameongozwa na Mtaliano", huku akimpongeza Ranieri na klabu yake ya Leicester City kwa kushinda taji hilo.

Ranieri, 64, amekuwa gumzo katika dunia ya michezo kwa mafanikio yake, akiiongoza Leicester kubeba ubingwa huku wakiwa na mechi mbili mkononi kufuatia Tottenham Hotspur kutoka sare ya 2-2 nyumbani kwa Chelsea.

Ranieri alikabidhiwa mikoba King Power Stadium kiangazi kilichopita baada ya Foxes kuweza kuepuka kushuka daraja karibu na mwisho wa msimu uliopita.

Licha ya kampuni za kamari kuipa Leisester 5,000-1 kuweza kuibuka bingwa mwanzo wa msimu, Ranieri amewaonyesha kuwa walikuwa wakifikiri sivyo, na kujizolea sifa kutoka kila kona na kupata heshima kubwa nyumbani kwao Italia.



Comments