LEICESTER City imetwaa kwa mara ya kwanza            taji la Premier League bila kushuka dimbani baada ya mechi            kati ya Chelsea na Tottenham kumalizika kwa sare ya 2-2,            lakini hiyo haikuwa historia pekee iliyoandikwa Stamford            Bridge Jumatatu usiku.
        Bali matokeo hayo yalikwenda sambamba na            Spurs kuandika historia ya kuwa timu ya kwanza katika historia            ya Premier League wachezaji wake tisa kulimwa kadi za njano            katika mechi moja na kushangaza zaidi kwa kukosekana hata            mmoja wa kutolewa nje kati yao!
        Kutoka dakika 27 hadi 51 tayari nyota wanne walilimwa            kadi, mmoja mwingine akipewa kadi kati ya mabao mawili ya            Chelsea na wanne zaidi baada ya Eden Hazard kufunga bao la            kusawazisha dakika 83, ambapo watatu kati yao katika dakika za            majeruhi.
        Nyota wa Spurs waliolimwa kadi za njano ni Kyle Walker            (dk 27), Jan Vertonghen (dk 38), Danny Rose (dk 45), Erik            Lamela (dk 51), Christian Eriksen (dk 70), Eric Dier (dk 88),            Harry Kane (dk 90), Moussa Dembele (dk 90) na Ryan Mason (dk            90).
        
Comments
Post a Comment