STAA Thiago              Alcantara ameelezea dhamira yake ya kubaki Bayern Munich              licha ya kuendelea kuwepo na tetesi zinazodai kwamba              ataondoka na kocha wake, Pep Guardiola atakapokwenda              Manchester City.
        Guardiola ndie              aliyempeleka Thiago Bayern akitokea Barcelona wakati kocha              huyo alipoanza kuinoa klabu hiyo ya Allianzarena mwaka 2013              na sasa kuna tarifa zinazodai kwamba anataka kuwa na staa              huyo mwenye umri wa miaka 25 kwenye kikosi chake kipindi              atakapoanza kibarua chake kipya katika michuano hiyo ya Ligi              Kuu England.
        Hata hivyo,              mapema mwaka huu Thiago alikanusha taarifa hizo za kwamba              anataka kuitema klabu hiyo ya mabingwa wa Ligi ya Bundesliga              na tena juzi kupitia katika mitandao ya kijamii akarudia              kauli yake hiyo ya kwamba ataendelea kuitumikia.
        "Nawashukuru kwa              msaada wenu, tutaonana msimu ujao," aliandika kupitia              mtandao wake wa Twitter.
        
Comments
Post a Comment