STAA wa zamani wa              Manchester United, Paul Scholes ni kama anampigia debe nyota              mwenzake wa zamani, Ryan Giggs, baada ya kusema kwamba ana              matumaini atakuwemo kwenye jopo la wafanyakazi wa Jose              Mourinho wakati atakapokuwa akiinoa klabu hiyo ya Old              Trafford.
        Mourinho ndie              aliyemrithi Louis Van Gaal katika kitimoto cha klabu hiyo ya              Old Trafford baada ya Mholanzi huyo kufukuzwa zikiwa ni siku              mbili tangu aiwezeshe Manchester United kutwaa ubingwa wa              Kombe la FA.
        Giggs alikuwa              msaidizi wa Van Gaal katika kipindi cha miaka miwili na              alikuwa akitajwa kuwa ndie angekabidhiwa timu hiyo mwaka              2017 ambao kocha huyo wa zamani wa Barcelona alikuwa              amepanga kuondoka lakini Mourinho anadaiwa kuwa ataajiri              wafanyakazi wake akiwemo mshirika wake wa karibu, Rui Faria.
        Hali hiyo ndiyo              inayoweka shakani kibarua cha Giggs na huku ripoti nyingine              zikidai kwamba mshindi huyo mara 13 wa mataji ya Ligi Kuu              anaweza kutafuta kibarua kwingine.
        
Comments
Post a Comment