Louis van Gaal            anaonekana kama vile anakiri kuwa muda wake wa kuwa kocha wa            Manchester United umefika ukingoni baada kuondoka London huku            akiwaambia waandishi wa habari 'it's over' (imekwisha/imefika            mwisho).
        Licha ya kushinda            taji la FA kwa ushindi wa  2-1 katika mchezo ulioenda hadi            'extra time' dhidi ya Crystal Palace siku ya Jumamosi, hatma            ya kocha huyo iliingia mashakani kwa mara nyingine tena muda            mfupi tu baada ya mchezo huo uliochezwa Wembley. 
        Mwandishi wa Sky            Sports James Cooper aliyekuwepo nje ya hotel ya Hilton            katikati ya London walikofikia Manchester United, anafichua            kuwa Van Gaal alipoulizwa kuhusu hatma yake alijibu: "No, no.            It's over!".
        BBC imedai Jose            Mourinho atatangazwa kuwa kocha mpya wa Manchester United            ndani ya siku chache zijazo.
        Louis van Gaal                    akiondoka jiji la London kurejea Manchester baada ya                    mchezo wa fainali ya FA
              
Comments
Post a Comment