SABABU 5 ZINAZODHIHIRISHA MARTIAL NI MCHEZAJI MKUBWA DUNIANI


SABABU 5 ZINAZODHIHIRISHA MARTIAL NI MCHEZAJI MKUBWA DUNIANI

Martial 2

Ni ukweli usiofichika kwamba Anthony Martial ni moja ya wachezaji waliopata mafanikio makubwa sana katika msimu huu wa EPL.

Kinda huyo wa raia wa Ufaransa alijiunga na Manchester United kwa ada ya paundi milioni 36 akitokea klabu ya Monaco ya Ufaransa.

Watu wengi waliutilia shaka uhamisho wake, wakidai kwamba amegharimu kiasi kikubwa cha fedha ukilinganisha na umri wake bila ya kusahau changamoto zilizopo Ligi Kuu England. Lakini haikuchukua hata mwezi Martial kuwaziba midomo walimtilia mashaka.

Kwa ufupi tu, tuangazie takwimu ambazo zinathibitisha dhahiri shahiri kwamba Martial tayari ni mchezaji mkubwa kwenye Ligi ya England.

  1. Amekuwa mfungaji bora wa Man United katika msimu wake wa kwanza
Anthony Martial ndiye kinara wa ufungaji katika kikosi cha Manchester United. Amefunga magoli 18 na kutoa pasi za magoli 9, na kumfanya awe mfungaji bora wa United msimu huu.
  1. Amevunja rekodi

Martial 4

Amevunja rekodi ya kuwa mchezaji ghali zaidi kijana kuwahi kusajiliwa katika historia ya klabu ya Manchester United. Amekuwa mchezaji wa kwanza chini ya miaka 20 kununuliwa kwa paundi milioni 36.

3. Amefunga goli la kihistoria

Alifunga goli la 1000 kwa Manchester United katika dimba la Old Trafford. Ni bahati ya kipekee kwake.
  1. Uwezo wa kuzoea mazingira kwa haraka
Yamkini amekuwa ni mchezaji pekee wa United kufunga katika michezo yake mitatu ya mwanzo.
  1. Anaweza kuwa na ubora zaidi ya Cristiano Ronaldo
Anthony Martial-tuzo
Licha ya kuwa kwenye ubora wa hali ya juu, lakini ikumbuwe kwamba ilimchukua takriban mechi 39 Ronaldo kufunga magoli matano tu, huku Martial akiwa amefanya hivyo ndani ya mechi 9 tu.


Comments