ROBERT LEWANDOWSKI NJIANI KUELEKEA REAL MADRID



ROBERT LEWANDOWSKI NJIANI KUELEKEA REAL MADRID
After bagging 30 goals for Bayern Munich last season he            became the first non-German to hit that figure
Robert Lewandowski anaweza kuwa njiani kuondoka Bayern Munich kiangazi hiki baada ya wakala wake kubainisha kuwa kuna maongezi yameanza ya mchezaji huyo na Real Madrid.

Mshambuliaji huyo ambaye kwa sasa yupo na timu ya taifa ya Poland inayojiandaa na michuano ya Euro 2016, alikuwa nguzo kuu katika kuiwezesha Bayern kutwaa taji la Bundesliga kwa mwaka wa nne mfululizo akifunga magoli 30 na kuwa mchezaji wa kwanza asiye raia wa Ujerumani kufanya hivyo.

Baada ya kutumia muda wake mwingi kucheza soka la kulipwa Ujerumani, nyota huyo mwenye umri wa miaka 27, hakufanya siri utashi wake kutaka kusaka changamoto mpya nje ya Bundesliga na sasa wakala wake Cezary Kucharski  anazidi kuchagiza hatua hiyo kwa kufichua kuwa Real Madrid tayari wamebisha hodi kusaka huduma ya mteja wake.
Robert Lewandowski has held                  talks over a switch to Champions League finalists Real                  Madird
Robert Lewandowski njiani kutua Real Madird




Comments