RAPHAEL VARANE KUIKOSA MICHUANO YA EURO



RAPHAEL VARANE KUIKOSA MICHUANO YA EURO
BEKI wa timu ya taifa ya Ufaransa, Raphael Varane ameachwa kwenye kikosi cha timu ya taifa ya nchi hiyo.

Varane hajajumuishwa kwenye kikosi kitakachoshiriki michuano ijayo ya Euro itakayoanza mwezi Juni kutokana na kusumbuliwa na majeraha ya nyama za paja. 

Pia nyota huyo wa klabu ya soka ya Real ameukosa mchezo wa fainali ya Kombe la klabu bingwa Ulaya uliopigwa leo kati ya timu yake na Atletico Madrid.


Mchezaji huyo atakuwa nje ya uwanja kwa muda wa wiki tatu hadi nne na nafasi yake kwenye kikosi cha taifa imechukuliwa na beki wa Adil Rami, mwenye umri wa miaka 30 anayechezea timu ya Sevilla ya nchini Hispania.


Comments