WACHEZAJI wa kigeni wa klabu ya Simba,            pamoja na mchezaji mzawa Mwinyi Kazimoto, wameikacha safari ya            klabu hiyo iliyokuwa ikienda mkoani Ruvuma kuvaana na Majimaji            ya Songea.
        Wachezaji waliokacha safari hiyo ni            Vincent Angban, Juuko Murshid, Emery Nimubona, Justice            Majabvi, Hamis Kiiza, Brian Majwega na Mwinyi Kazimoto. 
        Chanzo kikuu cha wachezaji hao kukacha            safari hiyo iliyofanyika leo kwa ajili ya mchezo wao wa 28 wa            Ligi kuu Tanzania Bara dhidi ya Majimaji ya Songea, ni            kutolipwa mishahara yao. 
        Ofisa habari wa klabu ya Simba, Haji            Manara, alisema kuwa sababu ya kuchelewa kuwapa mishahara            wachezaji wao inatokana na wadhamini wao Kampuni ya Bia            Tanzania (TBL) kuchelewa pia kuwapatia fedha za udhamini. 
         "Mfano            Mwinyi alikuwa hapatikani kabisa kwenye simu, lakini hawa            wengine walikataa kwenda sababu ya kutolipwa mishahara            yao"alisema Manara. 
        Licha ya kutaja wachezaji hao, kuna wachezaji ambao wameshindwa kwenda Songea kutokana na kuwa wagonjwa, ambao ni Raphael Kiongera, Jonas Mkude, Awadhi Juma na Ibrahim Ajib ambaye alionyeshwa kadi nyekundu Jumapili katika mechi ya ligi dhidi ya Mwadui FC

Comments
Post a Comment