Manchester City iko            mbioni kushinda vita vya kuwania saini ya kiungo mkongwe wa            Arsenal anayeelekea kutundika daluga.
        City inataka            kumnasa nyota huyo wa Hispania mwenye umri wa miaka 34 ili            akawe kocha msaidizi wa Pep Guardiola.
        Mara baada ya            mchezo wa mwisho wa Ligi Kuu baina ya Arsenal na Aston Villa,            Arteta aliweka wazi kuwa ana ofa tatu mkononi za benchi la            ufundi ikiwemo ya kwenda Machester City.
        Mikel              Arteta (katikati) akilia baada ya mchezo wake wa mwisho kwa              Arsenal Jumapili iliyopita 
        Mikel              Arteta akifarijiwa na wachezaji wenzake
          Ofa zingine za            ukocha usaidizi ambazo Arteta hakutaka kuzitaja zinahusishwa            na Arsenal na Tottenham, lakini inaaminika kuwa  tayari City            imepiga hatua kubwa mbele katika dili hilo.
        
Comments
Post a Comment