MICHAEL CARRICK KUONDOKA MANCHESTER UNITED ...ARSENAL YATAJWA KUMVIZIA


MICHAEL CARRICK KUONDOKA MANCHESTER UNITED ...ARSENAL YATAJWA KUMVIZIA
The            34-year-old was accompanied by his children, Jacey and Louise,            for the victory over Bournemouth
Michael Carrick anaamini Jumanne usiku katika uwanja wa Old Trafford, alicheza mchezo wake wa mwisho kwa Manchester United kwenye uwanja wao wa nyumbani.

Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 34 alisindikizwa na watoto wake, Jacey na Louise, wakati alipoiongoza United kuingia uwanjani kwenye mchezo wao wa mwisho wa Premier League msimu huu dhidi ya Bournemouth. 

Rio Ferdinand na Patrice Evra nao pia walisindikizwa na watoto wao katika mchezo wa mwisho Old Trafford, ishara inayoonyesha kuwa Carrick naye anaweza akatimka United baada ya fainali ya FA dhidi ya Crystal Palace Jumamosi huu.

United bado haijaonyesha nia ya kumbakiza Carrick kwa kile kinachoaminika kuwa inataka kuwekeza kwa vijana zaidi. Arsenal na Newcastle zinatajwa kuwania saini ya kiungo huyo iwapo ataachwa na Manchester United.
Midfielder Michael Carrick                  believes he has played his final game for Manchester                  United at Old Trafford
Kiungo Michael Carrick anaamini mwisho wake Manchester United  umewadia
Carrick is United's second                  longest-serving player after Wayne Rooney but hasn't                  been offered a new contract
Carrick (kushoto) na Wayne Rooney ndiyo watumishi wa muda mrefu waliosalia kwenye kikosi cha United


Comments