Michael Carrick            anaamini Jumanne usiku katika            uwanja wa Old Trafford, alicheza            mchezo wake wa mwisho kwa Manchester United kwenye uwanja wao            wa nyumbani.
        Kiungo huyo mwenye            umri wa miaka 34 alisindikizwa na watoto wake, Jacey na            Louise, wakati alipoiongoza United kuingia uwanjani kwenye            mchezo wao wa mwisho wa Premier League msimu huu dhidi ya            Bournemouth. 
        Rio Ferdinand na            Patrice Evra nao pia walisindikizwa na watoto wao katika            mchezo wa mwisho Old Trafford, ishara inayoonyesha kuwa            Carrick naye anaweza akatimka United baada ya fainali ya FA            dhidi ya Crystal Palace Jumamosi huu.
        United bado            haijaonyesha nia ya kumbakiza Carrick kwa kile kinachoaminika            kuwa inataka kuwekeza kwa vijana zaidi. Arsenal na Newcastle            zinatajwa kuwania saini ya kiungo huyo iwapo ataachwa na            Manchester United.
        Kiungo Michael Carrick              anaamini mwisho wake Manchester United  umewadia
        Carrick (kushoto) na              Wayne Rooney ndiyo watumishi wa muda mrefu waliosalia kwenye              kikosi cha United
        
Comments
Post a Comment