KINDA wa Manchester City raia wa Nigeria,            Kelechi Iheanacho amekiri kuwa amejifunza mengi kutoka kwa            kinda mwenzake wa Manchester United, Marcus Rashford msimu huu            na mkutakia mafanikio katika maisha yake ya soka.
        Makinda hao mastraika ambao wamekuwa            wakilinganishwa uwezo, wameng'ara msimu huu na klabu hizo            pinzani za Jiji la Manchester, wakionyesha ubora wa hali ya            juu katika kuzifumania nyavu.
        Rashford, Muingereza mwenye miaka 18            amepiga mabao saba katika mechi 16 akiwa na United, huku            Iheanacho mwenye miaka 19 akifunga 13 katika mechi 34            alizoichezea City.
        Iheanacho amevutiwa na            Rashford tangu alipoibuka Februari mwaka huu, na amekiri kuwa            amejifunza mengi kutoka kwake na anaamini atakuwa mchezaji            mkubwa Old Trafford.
        "Rashford ni kipaji kichanga cha hali ya juu. Ni            "mkubwa", madhubuti na anafanya maamuzi mazuri, hivyo nadhani            anaelekea kuwa mchezaji mzuri wa United miaka ijayo," alisema            Iheanacho kuliambia gazeti la Daily Mail.
        Akizungumzia kulinganishwa na            Rashford, alisema ni changamoto nzuri kwa sababu inampa hamasa            na ujasiri zaidi wa kupambana.
        
Comments
Post a Comment