KIUNGO Mario Gotze amerejea mazoezini              katika timu ya taifa ya Ujerumani baada ya kupona tatizo              lake la kuvunjika mfupa wa ubavuni.
        Kutokana na majeraha hayo, kiungo huyo              mshambuliaji wa Bayern Munich alilazimika kuikosa mechi ya              fainali ya Kombe la Ujerumani DFB – Pokal, lakini juzi              akarejea kwenye kikosi cha Ujerumani kilichopo nchini Uswisi              kwa ajili ya kujiandaa na mechi mbili za maandalizi ya              fainali za Mataifa ya Ulaya (Euro 2016), dhidi ya Slovakia              na Hungary.
        Gotze alijikuta katika kipindi kigumu              Bayern katika muda wa mwisho wa Pep Guardiola kwenye klabu              ya Allianzarena na licha ya Carlo Ancelotti kuwa ndie              atakayeinoa kuanzia msimu ujao, kuna taarifa zinazodai              kwamba atakwenda kuungana na kocha wake wa zamani wakati              akiwa Borussia Dortimund, Jurgen Klopp anayeinoa Liverpool.
        Akizungumza kuhusu Gotze katika mkutano              wa waandishi wa habari juzi, kocha wa timu ya taifa ya              Ujerumani, Joachim Roy alisema kwamba aliwasiliana na staa              huyo wiki iliyopita na akameleza kila kitu kuhusu hali ya              afya yake.
        
Comments
Post a Comment