MANCHESTER United sasa inasubiri miujiza kumaliza            katika nafasi ya nne katika Ligi Kuu ya England baada ya            kukubali kichapo cha bao 3-2.
        Kabla ya mchezo wa huo wa kiporo uliochezwa Jumanne            usiku kwenye dimba la Upton Park, United ilikuwa na  matumaini            ya kumaliza katika nafasi ya tatu, lakini sasa imebakiwa na            nafasi finyu ya kushika nafasi ya nne.
        United yenye pointi 63 sasa italazimika kushinda mchezo            wake wa mwisho dhidi ya AFC Bournemouth Mei 15 halafu iombe            Manchester City yenye pointi 65 ifungwe na Swansea City,            kinyume na hapo, klabu hiyo ya Old Trafford itajikuta            ikiambulia nafasi ya kucheza Europa League msimu ujao huku            Champins League ikiota mbawa kwao.
        West Ham ilikuwa ya kwanza kufunga katika dakika ya 10            kupitia kwa Diafra Sakho bao lililodumu hadi mapumziko.
        Anthony Martial akaifungia United mabao mawili katika            dakika ya 58 na 72 na kuifanya West Ham ikicharuke na kupata            magoli yaliyokuja dakika ya 76 na 81 yaliyofungwa na Michail            Antonio na Winston Reid.
        
Comments
Post a Comment