MATAJIRI wa jiji la Manchester, Manchester City,            wameweka jina la mlinzi wa Bayer Leverkusen, Lukas Boeder            katika orodha ya wachezaji wanaowawania katika usajili wa            majira ya kiangazi.
        Kwa mujibu wa Daily Mail, City inapambana na klabu            nyingine nyingi zinazowania saini ya mlinzi huyo, ikiwemo            Barcelona.
        Lakini City imetajwa kuwa katika mkakati mzuri wa            kumnasa Rolfes ikiwa ni azma ya kukiimarisha kikosi cha msimu            ujao.
        Boeder amekuwa katika kiwango kizuri kwa miaka miwili            iliyopita na kuwa tegemeo katika kikosi cha Bayer Leverkusen.
        Mlinzi huyo amekuwa miongoni mwa wachezaji wa mwanzoni            kuingia katika rada za usajili wa Manchester City inayopanga            kupambana kwa ajili ya kurejea katika mafanikio makubwa msimu            ujao.
        Katika kuhakikisha wanafanikisha azma hiyo, City            imekuwa ikimfuatilia Boeder katika baadhi ya mechi ambazo            Leverkusen inacheza ndani ya Bundesliga.
        Mawakala wa City wamekuwa wakisafiri mara kwa mara hadi            nchini Ujerumani kwa ajili ya kujiridhisha na kiwango cha sasa            cha mlinzi huyo.
        
Comments
Post a Comment