BOSI wa Matajiri wa Jiji            la Manchester, Manchester City, Manuel Pellegrini wala hana            haja ya mustakabali wake wa ama kubaki au kuondoka.
        Katika              kujiaminisha kuwa bado ana nafasi ya kubaki, ndio kwanza              ameanza kupanga safu ya usajili wa dirisha la majira ya joto              kwa kusaka saini ya beki wa kati, Lukasz Piszczek.
        City imekuwa              katika mbio za kumsainisha nyota huyo kutoka Borussia Dortmund ya            Ujerumani kwa dau la pauni 35 mil.
        Hatua ya City              kutaka kumwita kundini mlinzi huyo ni kutokana na mkakati              wake wa kuendelea kusuka kikosi imara cha kuipa mataji              klabu.
        City iliyoshindwa              kutetea taji la premier msimu uliopita, ilimweka katika              wakati mgumu kocha Manuel Pellegrini na sasa imepanga              kuingia sokoni kusajili nyota kadhaa walio bora.
        Akinukuliwa              Pellegrini alisema: "Lukasz ni kati ya wachezaji muhimu kwa              sasa walio katika kiwango cha juu na ana kipaji cha kuweza              kucheza katika klabu yoyote kubwa hivyo City haipaswi              kumuacha."
        "Ana sifa moja              kubwa, nayo ni uwezo wake wa kuwakabili washambuliaji wa              timu pinzani na anajua kujipanga hasa katika mazingira              magumu."
        "Kizuri ambacho              ni sifa yake ya ziada ni kwamba ni mzuri katika kupanga safu              ya ulinzi, hivyo ni mtu muhimu kwa sasa katika kiwango cha              soka la dunia," alizungumza Pellegrini na kunukuliwa na The              Goal. 
        "Sikuwahi              kumshawishi kwa kiasi kikubwa, lakini ninatambua vyema uwezo              alionao ambao ni muhimu kwetu kma klabu itafanya jitihada              kumpata na kuimarisha safu ya ulinzi."
        "Kama atafanikiwa              kutua kwetu nitajisikia furaha ya kupitiliza kwasababu ndoto              ya fikra zangu itakuwa imetimia."
        "Hakuna jambo la              siri ukiwa unamalizana na mchezaji bora wa kiwango chake. Ni              vyema kuwa na wachezaji wanne ama watano katika kikosi              utakuwa umejihakikishia kikosi bora."
        "Kama unaweza              kusema lililo kweli ni kwamba ndani ya kikosi chetu              tulihitaji wachezaji wa mfano wake ambapo ninaamini anacheza              vyema na Vicent Company."
        Manchester City              imepanga kutumia kiasi kikubwa cha fedha kwa ajili ya              kufanya usajili wa dirisha la Januari, huku azma ikiwa ni              kurejesha heshima ya kutwaa ubingwa premier ambao msimu huu              umechukuliwa na Chelsea.
        
Comments
Post a Comment