LUIS SUAREZ ATOA KAULI NZITO KUHUSU LIONE MESSI


LUIS SUAREZ ATOA KAULI NZITO KUHUSU LIONE MESSI
Barcelona forward Luis            Suarez has had a superb season and is one the verge of 60            goals for the campaign

KUNA kauli moja amezungumza Luis Suarez kuwa awali hakuwa na ndoto ya kuweza kucheza vyema akiwa katika kikosi kimoja na nyota wa dunia, Lionel Mess.

Lakini tangu akiwa Barcelona na kumudu kupewa majukumu ya kucheza kama mshambuliaji wa kati, amefarijika na hatua ya kiwango chake cha sasa.

Alisema, kabla ya kujiunga na Barca akitokea Liverpool mwaka 2014 hakutarajia kucheza katika jukumu alilonalo Messi, ingawa kwa sasa amekiri kufanikiwa.

Suarez kwa sasa amepachika mabao 40 katika mechi 35 ambazo alipangwa msimu huu na kuingia katika orodha ya wachezaji walio na magoli mengi akichuana na Cristiano Ronaldo wa Real Madrid.

Kwa nyakati tofauti, Messi amekuwa nje ya kikosi cha Barca kwa sababu mbalimbali, ikiwemo kuwa majeruhi, lakini Suarez amekuwa akichukua nafasi yake na kucheza kama mshambuliaji wa kati.

"Nimekuwa nikipangwa kama namba tisa wakati Messi hayupo ama hata akiwepo tumekuwa tukicheza kwa kubadilishana wakati mchezo ukiendelea. Hii ni hatua ya kujivunia," anaeleza Suarez

"Kucheza katika mfumo wa kujiamini na kupokezana kumeisaaidia timu kutomtegemea mchezaji mmoja katika idara ya ushambuliaji, ndio maana utatukuta tunacheza kwa kupichana."

"Ninaweza nikawa mimi, baadae Messi na kisha Neymar, wote tumekuwa tukipangwa kulingana na aina ya mchezo na tumekuwa katika mfumo mzuri siku zote," alisisitiza Suarez na kuongeza."

"Nimekuwa nikiwaambia kuwa watoto wangu kuwa ninacheza katika kikosi kimoja na mchezaji nyota duniani na ni jambo la kihistoria. Hii ni bahati na jambo la kujivunia."


Suarez alizungumzia kwa mara nyingine tukio la kung'ata Giorgio Chielini katika tukio lililofanyika wakati wa fainali za Kombe la Dunia mwaka 2014 nchini Brazil na kuliita ni jambo la kibinaadamu lisilopendeza.


Comments