Njozi za kocha Jurgen Klopp kutwaa taji la Ulaya katika            msimu wake wa kwanza Liverpool, zimeota mbawa baada ya timu            hiyo kulambwa 3-1 na Sevilla katika fainali ya Europa League.
        Liverpool ilikuwa ya kwanza kupata bao kunako dakika ya            35 kupitia kwa Daniel Sturridge, lakini Sevilla wakachomoa            dakika ya 46 kwa bao la  Kevin Gameiro.
        Coke akaifungia Sevilla mabao mawili ya haraka haraka            dakika ya 64 na 70 yaliyotosha kuimaliza Liverpool.
        Fainali hiyo ilipigwa kwenye uwanja wa St. Jakob Park            huko Basle, Switzerlandna            hiyo inakuwa ni mara ya tatu kwa Sevilla ya Hispania kutwaa            taji hilo.
        Daniel            Sturridge akishangilia bao pekee la Liverpool
        
Comments
Post a Comment