LIVERPOOL SAWA NA NGOMA YA KITOTO …YAPIGWA 3-1 NA SEVILLA, KOMBE LAENDA HISPANIA


LIVERPOOL SAWA NA NGOMA YA KITOTO …YAPIGWA 3-1 NA SEVILLA, KOMBE LAENDA HISPANIA
Liverpool keeper Simon            Mignolet flails as Gamiero meets an excellent cross from            Mariano to net from close range
Njozi za kocha Jurgen Klopp kutwaa taji la Ulaya katika msimu wake wa kwanza Liverpool, zimeota mbawa baada ya timu hiyo kulambwa 3-1 na Sevilla katika fainali ya Europa League.

Liverpool ilikuwa ya kwanza kupata bao kunako dakika ya 35 kupitia kwa Daniel Sturridge, lakini Sevilla wakachomoa dakika ya 46 kwa bao la  Kevin Gameiro.

Coke akaifungia Sevilla mabao mawili ya haraka haraka dakika ya 64 na 70 yaliyotosha kuimaliza Liverpool.

Fainali hiyo ilipigwa kwenye uwanja wa St. Jakob Park huko Basle, Switzerlandna hiyo inakuwa ni mara ya tatu kwa Sevilla ya Hispania kutwaa taji hilo.
The England              international celebrates scoring opener with with his now              customary dance moves
Daniel Sturridge akishangilia bao pekee la Liverpool


Comments