STRAIKA Lionel              Messi amesema kwamba anavyoamini timu ya taifa ya Argentina              ndiyo inayostahili kutwaa ubingwa wa michuano ya Copa              America Centenario itakayofanyika mwezi ujao nchini              Marekani.
        Argentina ilikosa              taji hilo mwaka jana kwa mikwaju ya penati dhidi ya Chile,              ikiwa ni takribani mwaka mmoja baada ya kuchapwa na              Ujerumani katika mechi ya fainali za Kombe la Dunia dhidi ya              Ujerumani zilizofanyika nchini Brazil.
        Vigogo hao wa              soka uknada wa Amerika Kusini wameshatinga mara tatu kati ya              nne za fainali hizo za Copa America lakini ikajikuta              ikiishia kuwa mshindi wa pili na haijawahi kutwaa taji hilo              tangu mwaka 1993.
        Hata hivyo Messi              sasa ni wakati wa Argentina kuonja ladha ya ushindi wa taji              hilo, ikiwa ni baada ya kuka muda wa miaka 23 bila kutwaa              taji lolote kubwa.
        "Tutajaribu              kufanya kila tuwezalo ili tutwae Kombe la Copa America,              kwasababu kwetu sisi ni muhimu mno," staa huyo wa Barcelona              aliuambia mtandao wa Sports Illustrated.
        "Cha muhimu zaidi              ni kwamba ni muda mrefu tangu Atrgentina ishinde taji lolote              na jambo hilo lilikaribia kumalizika wakati wa fainali za              Kombe la Dunia na michuano ya mwaka jana ya Copa America,"              aliongeza nyota huyo.
        "Nadhani              tunastahili kuwa mabingwa wa mashindano hayo muhimu,"              aliongeza tena staa huyo.
        Argentina itaanza              michuano hiyo kwa mechi ya kulipiza kisasi dhidi ya              watakayokutana nao kwenye fainali dhidi ya Chile Juni 6,              mwaka huu, kabla ya kuwavaa wapinzani wake katika kundi hilo              D, Panama itakayokutana nayo Juni 10 na siku nne baadaye              dhidi ya Bolivia.
        
Comments
Post a Comment