Hatimaye John Terry            amesaini mkataba mpya Chelsea utakaomwezesha kukipiga Stamford Bridge kwa mwaka mmoja zaidi.
        Terry ambaye            alikuwa njiani kutundika daluga, sasa atakuwa nafasi ya            kuongeza idadi ya michezo 703 aliyoichezea Chelsea aliyojiunga            nayo miaka 22 iliyopita.
        Habari hizi            zinaondoka kabisa ukungu uliotanda juu ya hatma ya nahodha            huyo mwenye umri wa miaka 35 ambaye alionekana kama anataka            kutupiwa virago vyake.
        Mwezi Januari Terry            alifichua kuwa klabu  haikuwa na nia yoyote ya kurefusha            mkataba wake, hali iliyoonyesha kuwa ndoa ya beki huyo na            Chelsea inaelekea ukingoni.
        Nahodha wa Chelsea John              Terry ameongezewa mwaka mmoja wa kubakia Stamford Bridge
        
Comments
Post a Comment