JOHN TERRY ASAINI MKATABA MPYA WA MWAKA MMOJA CHELSEA



JOHN TERRY ASAINI MKATABA MPYA WA MWAKA MMOJA CHELSEA
Terry will add to his 703              appearances for his boyhood club after agreeing new terms              with Chelsea this week
Hatimaye John Terry amesaini mkataba mpya Chelsea utakaomwezesha kukipiga Stamford Bridge kwa mwaka mmoja zaidi.

Terry ambaye alikuwa njiani kutundika daluga, sasa atakuwa nafasi ya kuongeza idadi ya michezo 703 aliyoichezea Chelsea aliyojiunga nayo miaka 22 iliyopita.

Habari hizi zinaondoka kabisa ukungu uliotanda juu ya hatma ya nahodha huyo mwenye umri wa miaka 35 ambaye alionekana kama anataka kutupiwa virago vyake.

Mwezi Januari Terry alifichua kuwa klabu  haikuwa na nia yoyote ya kurefusha mkataba wake, hali iliyoonyesha kuwa ndoa ya beki huyo na Chelsea inaelekea ukingoni.
Chelsea captain John Terry                  has signed a new one-year contract with the Stamford                  Bridge club
Nahodha wa Chelsea John Terry ameongezewa mwaka mmoja wa kubakia Stamford Bridge


Comments