JACK Wilshere              amemshambulia kocha Arsene Wenger kwamba anamuua kwa              kumchezesha katika nafasi isiyo yake klabuni Arsenal.
        Kiungo huyo, 24,              amekuwa akichezeshwa katika kiungo cha pembeni kwenye klabu              yake, lakini amekuwa akicheza kati zaidi katika timu ya              taifa ya England.
        "Klabuni Arsenal              nimekuwa nikicheza pembeni, eneo ambalo si langu," Wilshere              alisema.
        "Mimi si winga              lakini Roy (Hodgson), anaonekana kuwa na imani nami              kunitumia katika eneo la kati, hivyo nina furaha katika              hilo."
        Kocha wa timu ya              taifa ya England, Hodgson amemwita Wilshere katika kikosi              cahe cha awali cha wachezaji 26 kuelekea fainali za mataifa              ya Ulaya na anatarajiwa kuwemo katika wakali 23 watakaoenda              Ufaransa.
        Wilshere amecheza              mechi tatu tu msimu mzima Arsenal wakati akipambana kurejea              uwanjani kufuatia kuumia mguu, lakini Hodgson alidhamiria              kumwita taifa licha ya kutocheza kiasi cha kutosha.
        
Comments
Post a Comment